• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Ndalichako Asema Kila Kitu Kimekamilika Serikali ya Watu wa China Yatakiwa Kuanza Ujenzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi Mkoani Kagera

Imewekwa : January 28th, 2019

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako afanya ziara ya siku moja Kagera na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Vyuo vya Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Mkoani Kagera ili kuona ni hatua gani imefikiwa katika ujenzi huo ili vianze au viendelee kutoa huduma fanisi  kwa wananfunzi wanaohitimu Elimu ya Msingi na Kidato cha nne.

Profesa Ndalichako akiwa Mkoani Kagera Januari 26, 2019 alitembelea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa chuo cha Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) cha Mkoa wa Kagera katika Kijiji cha Burugo Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba kilometa chache kutoka Bukoba Mjini.

Profesa Ndalichako  alitembelea Burugo kwenda kujihakikishia kama jukumu la Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Serikali ya Mkoa wa Kagera limekamilishwa la kufikisha miundombinu ya Barabara, Maji na Umeme katika eneo hilo ili Serikali ya Watu wa China iweze kuanza ujenzi mara moja.

Mara baada ya kufika katika eneo la Burugo akiongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Deodatus Kinawiro aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera alikagua miundombinu ya Barabara, Maji na Umeme iliyofikishwa katika eneo hilo na Serikali na kusema kuwa sasa jukumu la Serikali limekamilika kwa asilimia 100% na kilichobaki ni Serikali ya Watu wa China kuanza ujenzi mara moja.

“Sisi Serikali ya Tanzania tumekamilisha kila kitu kilichotakiwa kwa upande wetu kilichobaki sasa ni Serikali ya Watu wa China kuanza ujenzi mara moja katika eneo hili ambapo ujenzi huo utagharimu jumla ya Shilingi bilioni 22.4 na chuo hiki kikamilika kitakuwa kinapokea jumla ya wanafunzi 800 wa fani mbalimbali za ufundi stadi kwa wakati mmoja.” Alifafanua Profesa Ndalichako.

Ikumbukwe kuwa Serikali ya Watu wa China mwaka 2015 ilihaidi kutoa shilingi bilioni 22.4 kwa ajili ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi na Rais Jakaya Kikwete akaagizachuo hicho kijengwe Mkoani Kagera. Ujenzi wa chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Mkoa wa Kagera unatarajia kuanza mwezi Mei 2019 mara baada ya taratibu za kusaini mikataba na manunuzi kukamilika.

Katika hatua nyingine Profesa Ndalichako alitembelea ujenzi na ukarabati wa Chuo cha Ufundi Stadi Wilayani Karagwe (Karagwe Development Vocational Training Center KDVTC) ambapo Serikali ilitoa Shilingi bilioni 4.6 ili Chuo hicho kiboreshwe miundombinu yake ya majengo na kujenga majengo mapya ili kiweze kukidhi viwango vya kupokea wanafunzi wengi zaidi.

Ujenzi wa Chuo cha KDVTC unaosimamiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na ngazi ya ujenzi ipo katika hatua ya msingi jambao ambalo lilimfanya Profesa Ndalichako kumwagiza Meneja wa Wakala wa Majengo Mkoa wa Kagera Mhandisi Salum Chanzi anayesimamia ujenzi huo kuhakikisha ujenzi unakamilika kwa muda uliopangwa wa mwaka mmoja ifikapo Julai 2019.

Aidha, katika hatua nyingine Profesa Ndalichako alitembelea Shule ya Sekondari Bukoba na kukagua majengo yaliyoezuliwa na upepo na upepo mkali usiku wa kuamkia tarehe 17.10.2018 pia majengo hayo yakiwa  yameathiriwa na Tetemeko la Ardhi la Septemba 10, 2016 na kuhaidi kuendelea na ufuatiliajia wa upatikaji wa fedha ili shule hiyo iweze kukarabatiwa na wananafunzi waliohamishiwa Shule za Sekondari Omumwani na Ihungo waweze kurejea na kuendelea na masomo katika Shule hiyo.

Kwa upande wa maendeleo ya Elimu katika Mkoa wa Kagera Profesa Ndalichako mara baada kupokea taarifa ya mkoa ya maendeleo ya elimu katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera aliupongeza uongozi na wananchi wa Mkoa wa Kagera kwa kuendelea kufanya vizuri na kuwa katika nafasi kumi bora za mwanzo katika mitihani mbalimbali.

Pia Profesa Ndalichako alisema kuwa mkoa unatakiwa kuzifanyia kazi haraka changamoto za miundombinu katika shule mfano uhaba wa matundu ya vyoo na mlundikano wa wanafunzi katika madarasa. “Chanagamoto ya vyoo inatakiwa kufanyiwa kazi haraka ukizingatiwa kuwa mkoa huu una mvua nyingi jambo ambalo linaweza kuhatarisha maisha ya watoto wawapo shuleni.” Alisisitiza Profesa Ndalichako.

Mkoa wa Kagera umeendelea kufanya vizuri katika matokeo mbalimbali na kuwa miongoni mwa mikoa kumi bora inayoshika nafasi za juu ambapo kwa miaka mitatu mfurulizo 2016, 2017, na 2018 Mkoa wa Kagera uliongoza kwa kushika nafasi ya kwanza Kitaifa kati ya mikoa 26 ya Tanzania Bara katika Mtihani wa Upimaji wa Darasa la Nne.

Matokeo ya Darasa la Saba Kitaifa mwaka 2016 Kagera ilishika nafasi ya 5, Mwaka 2017 nafasi ya 3 na mwaka 2018 nafasi ya 5 kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara. Katika Mtihani wa Upimaji wa Kidato cha Pili Kitaifa  kwa mwaka 2016 Kagera ilishika nafasi ya 4, Mwaka 2017 nafasi ya 6 na mwaka 2018 nafasi ya 7 kati ya mikoa 31 ya Tanzania Bara na Visiwani.

Aidha, Katika Matokeo ya Mtihni wa Taifa wa Kidato cha nne Mkoa wa Kagera kwa mwaka 2016 ilishika nafasi ya 3, Mwaka 2017 nafasi ya 9 na mwaka 2018 nafasi ya 8 Kitaifa kati ya mikoa 31 ya Tanzania Bara na Visiwani. Shule ya Kemebos iliyopo Manispaa ya Bukoba ilishika nafasi ya 2 Kitaifa mwaka 2018.

Pamoja na Mkoa wa Kagera kufanya vizuri katika matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2018 lakini Shule ya Sekondari Rwemondo iliyopo Wilayani Missenyi ilishika nafasi ya 4 kwa shule kumi za mwisho jambo ambalo linapelekea kengere kulia kwa uongozi wa Wilaya pia na Mkoa kuiangalia shule hiyo kwa jicho la tatu.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa